Thursday, January 26, 2023

TEUZI ZA RAIS SAMIA:Hofu rungu la Samia yatanda serikalini

 

Moshi/mikoani. Joto kwa wateule wa Rais linazidi kupanda baada ya mwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan kukamilisha kuunda safu ya uongozi wa juu wa chama hicho huku akiendelea kutimiza ahadi yake ya kuisuka upya Serikali.

Kufuatia ahadi hiyo ambayo haijulikani ukomo wake, baadhi ya wateule wanaishi kwa hofu na wasiwasi wakiwemo mawaziri, manaibu waziri, makatibu wakuu na manaibu wao, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, makatibu tawala wa mikoa na wilaya na wakurugenzi wa halmashauri.

Pia, wapo wakuu wa mashirika, wakala na taasisi mbalimbali ambao wamekuwa roho juu wasijue ukomo wa ahadi hiyo ya mkuu wa nchi.

Desemba 8 mwaka jana akiwa katika mkutano mkuu wa 10 wa CCM jijini Dodoma, Rais Samia alisema katika safari yake ya miaka miwili aliyoianza Machi 19, 2021 anahisi ana watu ambao mwendo wao hauendani na kasi ya Serikali yake ya awamu ya sita.

“Nawaomba sasa mnipe baraka zenu nikaipange Serikali pia. Nikaipange Serikali kwa jinsi ambavyo nahisi timu hii (ya CCM) tunaweza kwenda kuyatekeleza yale mliyoyasema hapa kwa vizuri zaidi,” alisema Rais Samia, kauli iliyoashiria mabadiliko makubwa yanakuja.

Wakati anaomba baraka hizo na kupewa na mkutano mkuu, Samia alikuwa hajamaliza kuunda Kamati Kuu na Sekretarieti, hatua ambayo aliikamilisha juzi kwa Halmashauri Kuu ya Taifa kuteua na kuthibitisha wajumbe wa Sekretarieti ya CCM huku wengi wa waliokuwemo wakiachwa.

Wajumbe wa sekretarieti waliosalia ni wawili tu, Daniel Chongolo anayeendelea na wadhifa wa katibu mkuu na Dk Frank Hawasi anayeendelea kuwa katibu wa NEC, (Uchumi na Fedha).

Walioteuliwa ni Anamringi Macha anayekuwanaibu katibu mkuu (Bara), Mohamed Said Dimwa (Naibu Katibu mkuu Zanzibar.

Pia katika safu hiyo, Sophia Mjema ameteuliwa kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi kuchukua nafasi ya Shaka Hamdu Shaka na Issa Haji Ussi katibu wa Ognaizesheni.


0 comments..:

Post a Comment